Home Simba SC KOCHA SIMBA : NITAMFANYA MORRISON AZIDI ‘KUKERA’ ZAIDI..!!!

KOCHA SIMBA : NITAMFANYA MORRISON AZIDI ‘KUKERA’ ZAIDI..!!!

 
MFARANSA wa Simba, Didier Gomes amewaambia wachezaji kwamba hataki mbwembwe nyingi za ‘anao anao’ yeye ni ‘unagusa unaachia twende’.

Gomes amesisitiza kwamba kikubwa anachotaka kwenye timu yake ni mpira wa kasi unaovutia na ushindi mnono.

Kocha huyo aliyetua Simba akitokea El Merreikh ya Sudan ambayo wapo nayo kundi moja la Ligi ya Mabingwa, ameapa kwamba kama wachezaji wakizoeana vizuri na kuelewa staili yake ya uchezaji timu zitapigwa nyingi.

Lakini amefurahishwa pia na ubora wa Bernard Morrison ambaye juzi alimpa dakika 25 akatupia bao mbili kwenye mechi dhidi ya Al Hilal.

Alisema anapenda soka la kumiliki mpira muda mwingi na kutengeneza nafasi za kufunga, huku akitaka wachezaji waongeze zaidi bidii mazoezini kuwa fiti kumudu kufanya vizuri kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.

Kwenye mechi yake na Al Hilal ya Sudan ambayo ni mtani wa El Merreikh alisema: “Niliamua kuanza na mfumo wangu wa 4-4-2, ambao Parfect Chikwende kucheza nyuma ya straika Meddie Kagere ili kuwa na uwezo wa kufunga muda wowote, lakini nyuma yao kuwa na wachezaji wengine wanne Clatous Chama, Larry Bwalya, Francis Kahata na Taddeo Lwanga ili kutawala na kumiliki mpira.

“Tulikuwa tunacheza vizuri wakati tukiwa na mpira na hata muda ambao hatakuwa nao na kwa muda wa siku tatu tuliofanya mazoezi wachezaji wangu wameonyesha kitu kikubwa ila tunatakiwa kuwa na mwendelezo.

“Jambo zuri kwangu kuanza kazi katika timu mpya na mechi ya kwanza tumeshinda mabao 4-1, dhidi ya Al Hilal ambao ni timu kubwa ya soka hapa Afrika na tulionyesha kiwango kizuri pia,” alisema Gomes ambaye Jumapili atakuwa na mtihani mwingine kwenye Super Cup dhidi ya TP Mazembe ya DR Congo.

KUHUSU MORRISON

“Hakuwa na muda mwingi wa kucheza kutokana na matatizo mbalimbali ambayo alikuwa nayo jambo ambalo limemsabisha utimamu wake wa kimwili, kuwa chini tofauti na wachezaji waliotumika mara kwa mara,” alisema.

“Morrison alicheza si zaidi ya dakika 30, katika mechi hiyo lakini alionyesha kiwango bora jambo ambalo litanipelekea kumpa nafasi ya kucheza zaidi kwani naimani anaweza kuonyesha kiwango bora zaidi ya kile.

SOMA NA HII  GOMES - MATOKEO YA JUMAMOSI YAMETUUMIZA MNO

“Namuona ni moja ya wachezaji ambao kama nikikaa nae chini na kumuondelea mambo mengine ambayo anayafanya ya nje ya uwanja atakuwa na kiwango bora zaidi ya alichoonyesha kwani anakipaji cha kuwa imara na bora na msahada kwa timu yetu,” alisema Gomes.

“Tangu nimefika katika mazoezi Morrison amekuwa mchezaji ambaye anayejituma na kutamani kucheza zaidi ndio maana ameonyesha kiwango kile ila nakwenda kumuandaa kwa kumpa mazoezi ya ufiti ili kuimarika zaidi,” aliongezea Gomes ambaye kwenye Ligi ya Mabingwa mechi ya kwanza anaanza na AS Vita ugenini mwezi ujao.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here