Home Simba SC SVEN AWAPA SIMBA MCHONGO WA KUWAMALIZA WAARABU KIMATAIFA

SVEN AWAPA SIMBA MCHONGO WA KUWAMALIZA WAARABU KIMATAIFA


ALIYEWAHI kuwa kocha mkuu wa klabu ya Simba, Sven Vandenbroeck amewapa mchongo waajiri wake hao wa zamani kwa kusema kama wanataka kufanya vizuri kimataifa, basi ni lazima wahakikishe wanakuwa na mshikamano na kutumia vizuri faida uwanja wa nyumbani kwani kundi walilopangwa ni gumu.

Sven aliyeiongoza Simba kwa misimu miwili akihudumu kwa nusu msimu kwenye kila msimu, alitangaza kuachana na Simba Alhamisi ya Januari 7, mwaka huu muda mfupi baada ya kuipeleka Simba hatua ya makundi kwa kwa kuiondosha FC Platinum ya Zimbabwe kwa jumla ya mabao 4-1.

Kocha huyo ambaye tayari amesaini mkataba wa miaka miwili ndani ya kikosi cha Far Rabat ya Morocco aliipa Simba mataji matatu ambayo ni; kombe la Ligi Kuu Bara 2019/20, kombe la FA 2019/20 na ngao ya jamii 2020/21.

Akizungumzia kundi ambalo wamepangwa waajiri wake hao wa  zamani, Sven amesema Simba wamepangwa kundi gumu kutokana na ubora wa timu zilizopangwa kwenye kundi hilo, lakini anaamini bado wana nafasi kubwa ya kufuzu hatua ya robo fainali.

“Ukiliangalia vizuri kundi ambalo Simba wamepangwa utagundua wazi kwamba wana kazi kubwa ya kufanya kutokana na ubora wa timu walizopangwa nazo, Al Ahly na AS Vita ni timu kubwa ambazo tayari zimefanya uwekezaji wa kutosha kwenye soka hivyo siyo rahisi kuwashinda licha ya kuwepo kwa kumbukumbu ya kufanya hivyo.

“Hata Al Merrikh sio wa kuwabeza, lakini naamini Simba bado wana nafasi ya kufuzu hatua ya robo fainali kama watakuwa na umoja na kutumia vizuri faida ya kucheza kwenye uwanja wao wa nyumbani, ni muhimu wakahakikisha pointi tisa za nyumbani zinasalia kwao kabla ya kufikiria ni jinsi gani waapata matokeo ya ugenini,” amesema Sven.

Akiwa na kikosi cha Simba Sven aliingoza timu hiyo kwenye michezo 55 akishinda mechi 39, amepoteza mechi sita na kutoa sare michezo kumi

SOMA NA HII  ACHANA NA KYOMBO ALIYETAMBULISHWA LEO...VIFAA VINGINE VIPYA KWA SIMBA HIVI HAPA...WEKA BANDO LA KUTOSHA...