Home news NAMUNGO:YALITOKEA NI SOMO KWETU, TUNARUDI TANZANIA KUJIPANGA

NAMUNGO:YALITOKEA NI SOMO KWETU, TUNARUDI TANZANIA KUJIPANGA


 KOCHA Mkuu wa Klabu ya Namungo, Hemed Morocco amesema kuwa mambo ambayo wamekutana nayo nchini Angola ni sehemu ya mchezo jambo ambalo linawafanya wajipange kwa ajili ya wakati ujao.

Namungo Februari 12 ilisafiri kutoka Bongo mpaka Angola kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wao wa Kombe la Shirikisho hatua ya 32 bora dhidi ya 1 de Agosto ya Angola.

Kilizuiwa Uwanja wa Ndenge wa Luanda Februari 13 kwa kile ambacho kilielezwa kuwa wachezaji wao watatu pamoja na kiongozi mmoja kukutwa na Virusi vya Corona.

Shirikisho la Soka Tanzania,(TFF) pamoja na Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya nje waliweka nguvu kwenye kufuatilia suala hilo ambapo majibu yalitolewa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kwamba mchezo wao ambao ulipaswa kuchezwa leo umefutwa na Kamati ya maadili italifuatilia suala hilo kwa ukaribu.

Kikosi cha  Namungo kinatarajiwa kurejea leo Februari 14 baada ya mchezo huo kufutwa.

Akizungumza Kocha Morocco amesema kuwa wanashukuru Mungu wapo salama ila yaliyotokea ni somo kwao.

 “Ni changamoto kwetu na ni somo pia hivyo hatuna la kusema kwa sasa,tunarejea kujipanga kwa ajili ya mechi zetu zijazo” ..

SOMA NA HII  KISA AUCHO...YANGA YAWAITA SIMBA MEZANI..MWENYEWE AFICHUA MKATABA WAKE..CHAMA APELEKWA YANGA...