Home Simba SC SAMATTA Sr :- HUYU MIQUISSONE HUYUU..!!

SAMATTA Sr :- HUYU MIQUISSONE HUYUU..!!


BABA mzazi wa Mbwana Samatta, anayekipiga Uturuki kwa mkopo wa mwaka mmoja akitokea Aston Villa ya England, ameshindwa kujizuia kwa Luis Miquissone wa Simba.

Mzee huyo anayejulikana kwa jina la Ally Pazi Samatta amesema Miqussone ni mchezaji hatari aliyetetemesha Misri kwa kiwango alichokionyesha timu yake ikicheza na Al Ahly.

Katika mchezo huo Simba iliibuka na ushindi wa bao 1-0, mchezo uliopigwa Uwanja wa Benjamin Mkapa, jambo ambalo limewapa ujasiri mashabiki wa Msimbazi kutembea kifua mbele.

Mzee Samatta amesema Miquissone ameonyesha maana halisi ya timu kusajili wageni wanaokusudiwa kuleta changamoto ya ushindani.

“Kimo chake kifupi hakikuzuia kuburuza ngome ya ulinzi ya Al Ahly, haogopi kupita katikati yao, huo ni ujasiri wa aina yake,” amesema na ameongeza kuwa;

“Miquissone hakuugopa kabisa mchezo ndio maana alicheza kwa kujiamini, wanatakiwa wachezaji wote wawe hivyo naamini wanaweza wakafanya kitu hata ugenini,”amesema.

Amesema amefunga bao la maarifa ambalo hata Al Ahly limewavutia na kuanza kutamani huduma yake.

SOMA NA HII  NEEMA ZAZIDI KUMIMINIKA KWA WACHEZAJI SIMBA...UONGOZI WATANGAZA 'SHANGWE' JIPYA LA KUFA MTU...

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here