Home Yanga SC KAZE: NINGEKUWA KWENYE BENCHI LA UFUNDI NINGEWAFUNGA SIMBA

KAZE: NINGEKUWA KWENYE BENCHI LA UFUNDI NINGEWAFUNGA SIMBA


 CEDRIC Kaze, aliyekuwa Kocha Mkuu wa Yanga amesema kuwa kama angekuwa bado ndani ya benchi la ufundi angewafunga Simba kwenye mchezo wa mzunguko wa pili.

Kaze alifutwa kazi Machi 7 baada ya kulazimisha sare ya kufungana bao 1-1 dhidi ya Polisi Tanzania kwenye mchezo uliochezwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid.

Yanga ilikuwa kwenye mwendo wa kusuasua ndani ya mzunguko wa pili ambapo ilicheza jumla ya mechi sita na kushinda moja, sare nne na ilipoteza mchezo mmoja kwa kufungwa mabao 2-1 dhidi ya Coastal Union, Uwanja wa Mkwakwani, Tanga ilikuwa Machi 4.

Kocha huyo amesema kuwa kwenye mchezo wa kwanza ambao alikiongoza kikosi hicho kusaka pointi tatu mbele ya Simba ndani ya Ligi Kuu Bara aliambulia sare ya kufungana bao 1-1 na kugawana pointi moja.

Mchezo wao wa mzunguko wa pili unatarajiwa kuchezwa Mei ambapo hatakuwa kwenye benchi la ufundi kwa kuwa ameshafungashiwa virago.

“Ingekuwa bado ningekuwa ndani ya benchi la ufundi la Yanga kuelekea kwenye mchezo wetu dhidi ya Simba Mei, ninaamini kwamba ningewafunga wapinzani wetu.

“Ninajua kwamba wengi hawawezi kuamini ila huo ni ukweli kwa sababu ninawajua wapinzani wetu vizuri na kwa namna ambavyo walikuwa bora walishindwa kuchukua pointi tatu kwetu.

“Mchezo wangu wa kwanza nilikuwa nina nafasi ya kupata pointi tatu ila aina ya wachezaji wangu walizidiwa mbinu mwishoni lakini kwa namna ambavyo nilikuwa nimewasoma basi mchezo wetu wa pili ningewafunga,”  anasema Cedric Kaze, aliyekuwa Kocha Mkuu wa Yanga.


SOMA NA HII  SIMBA YATAJA WACHEZAJI HATARI WA YANGA, SAIDO, KISINDA NDANI