Home CAF KOCHA AS VITA ATANGAZA KUIMALIZA SIMBA DAR

KOCHA AS VITA ATANGAZA KUIMALIZA SIMBA DAR


KOCHA mkuu wa AS Vita, Florent Ibenge amesema kuwa ili waweze kusonga mbele katika hatua ya robo fainali ya ligi ya mabingwa Afrika wanatakiwa kuibuka na ushindi katika michezo yao miwili iliyosalia ya ligi hiyo ikiwemo dhidi ya Simba.

AS Vita kwa sasa inashika nafasi ya 3 katika kundi A la ligi ya mabingwa mara baada ya kujikusanyia pointi 4 nyuma ya Simba waliona pointi 10 na Al Ahly ambao wamejikusanyia pointi saba.

Akizungumzia malengo yao katika michuano hiyo Ibenge amesema: “Tunatakiwa kushinda michezo yetu yote miwili iliyosalia dhidi ya Simba na Al Merrikh ili tuweze kusonga mbele katika hatua ya robo fainali.

“Matokeo tuliyopata hayajakuwa mazuri sana kwetu, lakini huu si muda wa kulaumiana tunachotakiwa kufanya ni kuhakikisha tunasonga mbele.

AS Vita wanatarajia kucheza na Simba ugenini Aprili 2, katika Uwanja wa Mkapa, Dares Salaam huku mchezo wa mwisho ukitarajiwa kufanyika kwao nchini Congo April 9, wakicheza dhidi ya Al Merrikh.

SOMA NA HII  MASHABIKI SIMBA WAMUANGUKIA KIBU