Home Simba SC GOMES: KWA KUWA SIMBA NI TIMU KUBWA ..MANULA ATABAKI..!!

GOMES: KWA KUWA SIMBA NI TIMU KUBWA ..MANULA ATABAKI..!!

 


SIKU za hivi karibuni kumekuwa na tetesi kwamba vigogo wa Sudan El Merrikh wanaiwinda kwa karibu sahihi ya kipa wa Simba Aishi Manula ambaye kwa sasa ameonekana kuwa na kiwango bora zaidi.

Gazeti la Mwanaspoti baada ya kuzipata tetesi hizo halikutaka kuziamini tetesi hizo bila uthibitisho ikabidi limtafute kocha mkuu wa Simba, Didier Gomes Da Rosa ambaye alifunguka ukweli na kusema Manula haondoki  klabuni hapo.

“Hizo ni habari za uongo, miezi mitatu iliyopita nilkuwa kocha wa Merrikh hivyo nawajua vizuri na mikakati yao na niwahakikishie mashabiki wa Simba kuwa huo ni uongo na Manula atabaki Simba.

Kwa sasa yupo kwenye kiwango kizuri na kila timu itahitaji kuwa na kipa kama yeye lakini kwakuwa na Simba ni timu kubwa, basi ataendelea kuwa hapa,” amesema Gomes.

Rekodi za sasa za Manula akiwa Langoni mwa Simba kwenye Ligi ya Mabingwa katika mechi tatu alizodaka ameruhusu bao moja tu jana Jumamosi dhidi ya As Vita Simba ikishinda 4-1.

Sambamba na Simba, pia Manula ni miongoni mwa wachezaji wenye mchango mkubwa katika timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kwan ndiye chaguo la kuwanza la kocha wa timu hiyo Kim Poulsen akiwaweka benchi mkongwe Juma Kaseja na Metacha Mnata.

SOMA NA HII  OKWA : MO DEWJI ALINITAKA NIJE SIMBA...KWA MAISHA YA HAPA KLABUNI...NI DENI TU...U