Home Simba SC ISHU YA MANULA, ONYANGO, TSHABALALA KUSEPA GOMES AFUNGUKA

ISHU YA MANULA, ONYANGO, TSHABALALA KUSEPA GOMES AFUNGUKA


 KOCHA Mkuu wa Simba, Mfaransa Didier 
Gomes amegoma kuona mastaa wake wakiondoka kwenye kikosi chake katika msimu ujao.

Kati ya mastaa wanaotajwa kuondoka Simba ni Mohammed Hussein ‘Zimbwe Jr’ anayedaiwa kusaini mkataba wa awali Yanga, Joash Onyango kwenda Orlando Pirates na Aishi Manula kuwaniwa na Mamelodi Sundowns zote za Afrika Kusini.

Zimbe Jr au Tshabalala hivi sasa  anaelekea kuwa mchezaji huru kwa kuwa mkataba wake unaelekea mwishoni.

“Muda wa usajili bado lakini nimeona vema kulizungumzia hili la wachezaji wangu wanaodaiwa kuondoka Simba mwishoni mwa msimu huu baada ya mikataba yao kumalizika.

“Binafsi sitakubali kuona wachezaji wangu hao wakiondoka kutokana na umuhimu mkubwa waliokuwa nao katika timu, kwani siku zote ni hatari kwa timu kufanya mabadiliko ya kikosi kwa kuwaondoa wachezaji walioipa mafanikio timu hasa msimu huu kimataifa.

“Lakini kingine sifahamu kuhusu kuondoka kwao, kitu kikubwa nitakachoweza kusema kuwa natamani kubakia na wote katika misimu mingine miwili hadi mitatu katika kutengeneza timu bora kwa ajili ya mafanikio ya timu, ” alisema Gomes.

Chanzo:Championi


SOMA NA HII  SIMBA NA CHAMA SASA ISHU IKAE HIVI TU