Home news KIBA ATUPIA BAO LA USHINDI RAMADHAN CUP

KIBA ATUPIA BAO LA USHINDI RAMADHAN CUP


 MWANAMUZIKI wa Bongo Fleva, Ali Kiba jana alifanikiwa kutimiza majukumu yake kwa umakini na kuifanya timu yake kushinda bao 1-0.

Kiba ambaye pia ni mchezaji wa mpira ni nahodha wa timu ya Bin Slum FC ambayo inashiriki Ramadhan Cup inayoendelea kila siku usiku, viwanja vya JK.

Wakati timu yake ikishinda bao 1-0 dhidi ya Asas Rangers Kiba ni yeye ambaye alipachika bao la ushindi kwa kichwa ndai ya 18 dk 27.

Mchezo mwingine ambao ulichezwa jana ulikuwa ni ule kati ya Silent Ocean ambao walishinda mabao 2-0 mbele  Scaba Scuba.

Kiba amesema:”Ninafurahi kuona kwamba nimefunga kwani kipaji kipo na uwezo tunao wa kufanya vizuri,”.


SOMA NA HII  SIKU 9 KABLA YA YANGA vs SIMBA...HAWA HAPA MASTAA WALIOPASHA ZAIDI MISULI YAO JOTO...