Home news SAA CHACHE KABLA KUCHEZA NA WAZAMBIA WENZAKE…BWALYA AFANYA MAAMUZI MAGUMU KISA SIMBA…

SAA CHACHE KABLA KUCHEZA NA WAZAMBIA WENZAKE…BWALYA AFANYA MAAMUZI MAGUMU KISA SIMBA…

 


Kiungo mshambuliaji Rally Bwalya, amesema atajitoa kuhakikisha anaisaidia Simba SC kufanya vizuri dhidi ya Red Arrows kesho ili kuingia hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika licha ya kucheza kwenye ardhi ya nyumbani kwao Zambia.

Bwalya amesema Simba ni waajiri wake na siku zote ataipa nafasi ya kwanza katika kila kitu kama mkataba wake unavyoeleza.

“Ninasikia furaha kucheza katika ardhi ya nyumbani, naipenda nchi yangu lakini nimekuja kikazi nitahakikisha naisaidia Simba kupata ushindi ili tuingie hatua ya makundi,” amesema Bwalya.

Akizungumzia mchezo wa leo Bwalya amesema itakuwa mgumu lakini tupo tayari kupambana kuhakikisha tunapata matokeo mazuri.

“Kama alivyosema kocha, mechi itakuwa ngumu, tunajua Red Arrows wataingia kwa nguvu kutafuta mabao lakini sisi ni Simba tutakuwa tayari kuwakabili,” amesema Bwalya.

SOMA NA HII  MCHAKATO WA KOCHA MPYA SIMBA..., BARBARA ATOKA NA HILI JIPYA...HAKUNA MTANZANIA HATA MMOJA ALIYEOMBA...