Home Habari za michezo BAADA YA ‘KUFYEKWA KININJA’ NA SIMBA…MORRISON KUTUA YANGA..CHIKO NAYE ‘SOON’ ATALIWA KICHWA...

BAADA YA ‘KUFYEKWA KININJA’ NA SIMBA…MORRISON KUTUA YANGA..CHIKO NAYE ‘SOON’ ATALIWA KICHWA YANGA…


Klabu ya Yanga huenda ikalazimika kuachana na mchezaji wao Chiko Ushindi endapo Benard Morrison atajiunga tena na Yanga.

Uongozi haujaridhishwa na kiwango Cha mchezaji huyo kutoka DRC aliejiunga nao dirisha dogo.

Habari za kuaminika ni kwamba Simba SC na Morrison wamekubalina kuvunja mkataba huku akiwa amebakiza miezi miwili tu Katika mkataba wake.

Simba SC wameachana na Morrison huku nafas yake huenda ikachukuliwa na mchezaji wa zamani wa Simba Luis Miquison aliejiunga na Al Ahly ambapo hajaonesha kiwango kizuri.

Al Ahly wapo tayari kumtoa kwa mkopo mchezaji huyo sharti tu Simba SC wakubali kumlipa mshahara wake Kamili na stahiki nyengine.

SOMA NA HII  BAADA YA KUONA WAMEZIDIWA KILA KITU ...BEKI SIMBA AKUBALI YAISHE...AKUBALI YANGA BINGWA MSIMU HUU..