Home Habari za michezo KUHUSU KUMSAJILI NTIBAZONKIZA MSIMU UJAO…KIGOGO SIMBA AANIKA YA NYUMA YA PAZIA…MCHEZO WOTE...

KUHUSU KUMSAJILI NTIBAZONKIZA MSIMU UJAO…KIGOGO SIMBA AANIKA YA NYUMA YA PAZIA…MCHEZO WOTE HUU HAPA…


Baada tetesi nyingi kuzagaa za kiungo Mrundi, Saidi Ntibanzokiza ‘Saido’ kutua Simba, uongozi wa timu hiyo umeibuka na kutamka hauna mpango wa kumsajili.

Hiyo ikiwa ni siku chache tangu Yanga itangaze kutomuongezea mkataba kiungo uliomalizika Juni 30, mwaka huu.

Mmoja wa mabosi wa Simba, amesema kuwa, ngumu kwao kumsajili mchezaji ambaye ameachwa na timu yake kutokana na utovu wa nidhamu.

Bosi huyo alisema, sababu nyingine ni umri na majeraha ambayo yanamuandama mchezaji huyo kila wakati akiwa Yanga kabla ya kutangaza kuachana naye.

Aliongeza kuwa, Bodi ya Wakurugenzi ya Simba, imepanga kufanya usajili bora na kabambe kujiandaa na msimu ujao, huku wakiwa katika mipango ya kukisuka kikosi kuwa imara kitakachoundwa na vijana wengi.

“Hizo tetesi tumeanza kuzisikia mara baada ya kiungo huyo kuachana na Yanga, hakuna ukweli wowote katika hilo, Simba hatuna mpango na Saido.

“Mchezaji aliyeshindikana na timu nyingine kutokana na tatizo la kinidhamu aje kusajiliwa Simba kwa sasa ni ngumu, kama uongozi tuna malengo makubwa.

“Malengo yetu ni kufika hatua ya nusu fainali au fainali ya michuano ya kimataifa, hivyo ni lazima tuwe na kikosi imara kitakachofanya vizuri msimu ujao,” alisema bosi huyo.

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally, alizungumzia usajili wa timu hiyo kwa kusema: “Tuna malengo makubwa na timu yetu kuelekea msimu ujao, tumepanga kufanya usajili mkubwa utakaotupa makombe, hivyo tusubiri muda ufike tuweke wazi.”

SOMA NA HII  SIMBA:...TUNAHUJUMIWA..BOSI AFUNGUKA MAMBO MAZITO...ATOA SIKU TATU...PABLO AJITIBULIA MWENYEWE..

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here